Uteuzi wa wajumbe wa Kamati ya TEITA kwa kipindi cha miaka mitatu 2022 -2025 kulingana na mabadiliko ya kifungu cha 5 cha sheria ya TEITI 2015.

NaCoNGO kwa kushirikiana na wadau toka Asasi za Kiraia (AZAKI/CSOs) zinazofanya kazi katika sekta ya Madini, Mafuta, na Gesi: Wanatangazia asasi zote zinazofanya kazi katika sekta ya Madini, Mafuta, na Gesi kuwa kutakuwa na zoezi la uchaguzi litakalofanyika tarehe 16.07.2022 jijini Dar es Salaam, katika ukumbi wa SeaShells Millenium Hotel kuanzia saa 3 asubuhi.

Tafadhali soma mwongozo wa uchaguzi na fuata maelekezo.

Kila asasi inayotimiza matakwa yaweza kuwa na mgombea mmoja na awasilishe maombi yake kwa anwani ifuatayo: info@nacongo.or.tz.

Maombi hayo yaambatanishwe na vifuatavyo:

  • Wasifu wa mgombea (CV)
  • Barua ya maombi ikieleza kifupi kwa nini unafaa kuwa mwakilishi (application letter)
  • Maelezo ya uwezo wa mgombea yasiyozidi kurasa mbili (personal capacity statement)

Maombi hayo yatumwe kabla ya tarehe 13.07.2022.

Washiriki wote wa uchaguzi wameombwa kujigharamia kufika jijini Dae es Salaam.

Kwa maelezo zaidi piga namba +255 (0) 767 544 560


Chanzo: NaCoNGO Website